Saturday 15 February 2020

MWANAMZIKI WA NYIMBO ZA INJILI ,CONNIE NASHIKA AWASHIRIKISHA CHRISTINA SHUSHO NA BONNY MWAITEGE - Bonyeza Star Tv



Connie Nashika
By Mkikuyu Mjaka

Mwanamziki Connie Nashika kutoka Kenya ,ambaye kwa sasa anatamba na kazi take mpya inayojulikana kama  MBARIKIWE ,amethibitisha kushirikiana na Muimbaji Christina Shusho wa Tanzania na pia vilevile Bonny Mwaitege kutoka nchi hiyo jirani.
Christina Shusho

Connie Nashika kupitia mitandao ya kijamii ameonyesha juhudi za kukamilisha kazi hizo mapema iwezekanavyo kwa minajili ya kuwapa mashabiki wake mziki mzuri na pia chakula cha roho kama mtumishi wa Mungu.
Msimamizi wa Connie ,Bwana Anthony Tambala pia ameweza kutuhakikishia kwamba haitachukua mda mrefu kabla tupate kazi hizo.

Bonny Mwaitege

No comments:

Post a Comment